Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Rais Magufuli Azindua Nyumba za Maafisa na Maaskari Magereza Ukonga Dar.

Posted on: January 23rd, 2020

RAIS Dkt. John Magufuli amelitaka Jeshi la Magereza Nchini kutathimini utendaji kazi wake kutokana na mwenendo usioridhisha wa jeshi hilo katika kutekeleza miradi mbalimbali inayopewa na Serikali.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Nyumba za Makazi ya Maafisa na Askari wa Jeshi hilo, leo (Alhamisi Januari 23, 2020) Ukonga Jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli alisema ameshangazwa na kasi isiyoridhisha ya utekelezaji wa miradi katika jeshi hilo licha ya kuwa na ukubwa wa kambi 129 nchini.

Akitolea mfano Rais Magufuli alisema Jeshi la Magereza lina jumla ya kambi 129 huku Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) likiwa na kambi 24 tu, lakini ameshangazwa na Magereza kujengewa nyumba za askari wake na JKT huku akishindwa kutumia nguvu kazi ya wafungwa walionao katika magereza mbalimbali nchini.

‘’Baada ya kutoa msamaha wa wafungwa zaidi ya 5000, sasa hivi katika magereza yote nchini kuna zaidi ya wafungwa 13,000 lakini tunashindwa kujenga nyumba za askari wetu, udongo kutoka kwa mungu tunao, hamna budi kujipanga na kuweka mikakati ili kuimarisha makazi ya askari ambao wanateseka’’ alisema Rais Magufuli.

Alisema mwezi Machi 2016 Serikali ilitoa kiasi cha Tsh Bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za askari magereza katika eneo la Ukonga Jijini Dar es Salaam na kutoa zabuni hiyo kwa Jeshi hilo pamoja na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), ambapo pamoja  kutumia miezi 27  walishindwa kuikamilisha kazi hiyo kwa kufikia asimilia 40-45 ya ujenzi wake.

Akifafanua zaidi alisema kutokana na kutoridhishwa na kasi hiyo, Serikali iliamua kuipa zabuni ya ujenzi wa mradi huo huo, Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ambapo ndani ya kipindi cha miezi 6 kuanzia mwezi Machi hadi Desemba mwaka 2019 ilikamilisha asilimia 55 ya ujenzi mradi huo kwa kutumia kiasi cha Tsh Bilioni 3 na kufanya mradi wote kutumia Tsh Bilioni 13.

Alibainisha kuwa ipo baadhi ya miradi mikubwa inayosuasua kutekelezwa na Jeshi hilo, ikiwemo Mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha Viatu katika Gereza la Karanga unaojengwa kwa ubia baina ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) na Jeshi la Magereza Nchini, ambao hadi sasa ujenzi wake hauridhishi kwani hakuna hata jengo moja lililokamilika hadi sasa.

‘’Mashine za kiwanda kile tayari zimewasili katika Bandari ya Dar es Salaam, lakini hadi sasa ni jengo moja tu lililofikia asilimia 49 ya ujenzi ndilo limesimama, sasa hizo mashine zitaenda kufungwa wapi, Mkataba wa Bilioni 9 umesainiwa, na ni mradi wenye ubia, kwa nini tunakwama’’ alisema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli aliipongeza JKT kutokana na kazi kubwa na nzuri inayofanya katika kusimamia na kutekeleza miradi mikubwa nchini ikiwemo ujenzi wa ukuta wa Mererani, Ujenzi wa Mji wa Serikali Dodoma na Ukuta wa Ikulu Dodoma wenye urefu wa Kilometa 27, na kulitaka Jeshi la Magereza kuiga mfano huo katika kujenga na kuboresha nyumba za makazi ya askari wa Jeshi hilo.

Kwa upande wake, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Hussein Mwinyi alisema Wizara yake inatambua juhudi kubwa zinazofanywa Rais Dkt. John Magufuli katika kuimarisha na kuboresha maslahi ya Maafisa na Askari wa Majeshi ya Vikosi vya Ulinzi na Usalama nchini ikiwemo ujenzi wa nyumba za makazi ya askari.

Waziri Mwinyi alisema katika Makazi hayo, yenye jumla ya ghorofa 12 zikiwemo ghorofa 8 za makazi askari na ghorofa 4 za makazi ya maafisa, zina jumla ya nyumba 172 zenye uwezo wa kutunza familia za maafisa na askari wa vikosi vya majeshi ya ulinzi na usalama.

Naye Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola alisema Wizara hiyo itaendelea kuhakikisha kuwa suala la ulinzi na usalama wa nchi linaendelea kusimamiwa kwa nguvu zote nchini kupitia vyombo vya dola ili kuwawezesha wananchi kushiriki kikamlifu katika shughuli za maendeleo.

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO