• Wasiliana Nasi
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Baruapepe za Watumishi
    • Malalamiko
TANZANIA INFORMATION SERVICES-MAELEZO
TANZANIA INFORMATION SERVICES-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo IDARA YA HABARI-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Serikali Kutekeleza Miradi 1,493 ya Maji Vijijini

Posted on: July 25th, 2018

Na: Lilian Lundo - MAELEZO, Dodoma.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli imetekeleza jumla ya miradi 1,493 ya maji vijijini kufikia Desemba, 2017 na ujenzi wa miradi 366 unaendelea kutekelezwa sehemu mbalimbali nchini.

Hayo yameelezwa leo, Jijini Dodoma na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa ahadi za Serikali.

"Mwaka 2017, Serikali iliendelea kutekeleza miradi ya maji vijijini kupitia programu ya kuendeleza sekta ya maji kwa lengo la kuongeza kiwango cha upatikanaji wa maji vijijini," amesema Dkt. Abbasi.

Aidha, amesema Serikali imetimiza ndoto ya kuendelea kulifufua Shirika la Ndege kwa kulera Boeing 787 Dreamliner na ndege nyingine mbili za C Series zinatarajiwa kufika Novemba mwaka huu wakati Boeing nyingine moja inatarajia kuwasili 2020.

"Manufaa ya ndege hizi yameanza kuonekana ambapo zinasaidia wananchi wengi kusafiri kwa haraka na kufanya biashara zao kwa haraka. Tangu tulete ndege hizi abiria wa ATCL wameongezeka kufikia 107,207 katika mwaka 2016/2017 kutoka 49,173 mwaka 2015/2016 ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 118," alifafanua Dkt. Abbasi.

Vile vile amesema katika Mwaka wa Fedha 2017/2018, Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilifanikiwa kukusanya jumla ya shilingi trilioni 15.5 kuanzia Julai 2017 hadi Juni, 2018 ikilinganishwa na shilingi trilioni 14.4 ambazo zilikusanywa katika kipindi kama hicho kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017, kiasi hiki ni sawa na ukuaji wa asilimia 7.5.

Dkt. Abbasi amesema, kutokana na utendaji makini wa Rais Magufuli na Serikali ya Awamu ya Tano kwa ujumla hata mashirika ambayo yalikuwa hayatoi gawio kwa Serikali sasa yanatoa.

"Juzi mmesikia zaidi ya shilingi bilioni 700 zimekusanywa kama gawio na mgawo wa asilimia 15 kutoka taasisi na mashirika ya umma na binafsi 43 na taarifa za sasa ni kuwa fedha hizi zitaongezeka hadi zaidi ya bilioni 800 ikiwa ni baada ya taasisi nyingine kuhamasika na hii ni ongezeko la asilimia zaidi ya 500," amefafanua Dkt. Abbasi.

Amesema kuwa, katika kutekeleza agizo la kuhamia Dodoma tayari watumishi 6,400 wamehamia mkoani humo.

Matangazo

  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Orodha ya Magazeti na Majarida ambayo Hayajahuisha Leseni ya Uchapishaji Serikalini February 05, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais Magufuli atunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa

    November 21, 2019
  • Rais Magufuli azindua Kitabu cha Maisha binafsi ya Rais Msaafu Benjamin Mkapa

    November 12, 2019
  • Rais Magufuli akutana na viongozi wa AALCO

    October 24, 2019
  • Afrika ni muhimu kwa Maendeleo ya Uchumi wa Dunia- Putin

    October 24, 2019
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: 25 Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@habari.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali ya Mwaka 2017/18
  • Tamko la Serikali kuhusu Matumizi ya Picha za Marais Wastaafu katika Sakata la Usafirishaji wa Mchanga wa Madini
  • Hotuba ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe akifungua mkutano wa 33 wa Jumuiya ya Mitaa Tanzania (ALAT)
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2019 GWF. Haki zote zimehifadhiwa.