Karibu!

Tunakukaribisha kwenye tovuti rasmi ya Msemaji Mkuu wa Serikali upate taarifa na habari sahihi zenye kuakisi malengo ya Serikali, Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 na matarajio ya Watanzania.

Mawasiliano

Tufuatilie

Na Baraka Messa – MAELEZO Serikali imesema Kongamano la Pili la Kimataifa la Kiswahili litakalofanyika jijini Paris, Ufaransa, kuanzia Julai 4 hadi 7, 2026, litakuwa jukwaa muhimu la kuitangaza Tanzania na Afrika kwa ujumla kupitia lugha ya Kiswahili, huku likitarajiwa kufungua fursa mpya za biashara, utalii na uwekezaji. Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa, amesema hayo jijini Dodoma wakati akizungumza kuhusu maandalizi ya kongamano hilo, akieleza kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha Kiswahili kinatumika kama lugha ya kimkakati katika kuchochea maendeleo ya uchumi. Jitihada za Serikali ni kuhakikisha Kiswahili kinatumika kama lugha ya kimkakati ili kiwe chachu ya kukuza biashara, kutangaza utalii na kuvutia wawekezaji kutoka sehemu mbalimbali duniani,” amesema Msigwa. Amesema Kiswahili kwa sasa si lugha ya mawasiliano pekee, bali ni rasilimali yenye fursa nyingi za kiuchumi, kielimu na kidiplomasia ambazo zinaendelea kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha maendeleo ya lugha hiyo duniani. Msigwa amesema mafanikio yaliyopatikana kupitia Kongamano la Kimataifa la Kiswahili lililofanyika Cuba yameongeza hadhi ya Kiswahili kimataifa, ambapo kwa sasa baadhi ya taasisi za elimu nchini Urusi na Ufaransa zimeanza kufundisha lugha hiyo. Pia amesema Kiswahili kimeanza kuingizwa katika mifumo ya kidijitali ikiwemo mitandao ya Kijamii, jambo linaloonyesha namna lugha hiyo inavyozidi kupata nafasi katika maendeleo ya teknolojia na ubunifu duniani. Kwa mujibu wa Msigwa, kongamano la Paris litahusisha tamasha kubwa la maonyesho ya Kiswahili, midahalo kuhusu tafiti na makala mbalimbali zinazohusu lugha hiyo pamoja na shughuli za kubadilishana uzoefu kati ya wadau kutoka mataifa mbalimbali. Takribani washiriki 1,000 wanatarajiwa kushiriki kongamano hilo, wakiwemo mabalozi, wawakilishi wa UNESCO, wataalamu kutoka vyuo vikuu, wafanyabiashara pamoja na taasisi mbalimbali za kitaifa na kimataifa. Amesema Serikali inaamini kuwa kupitia kongamano hilo, Kiswahili kitaendelea kujijengea heshima duniani na kuwa nyenzo muhimu ya kuimarisha ushirikiano wa kimataifa, kukuza biashara, utalii na uwekezaji kwa manufaa ya Tanzania na Afrika kwa ujumla. Mwisho

By Baraka Messa – MAELEZO Former Manchester United and England defender Rio Ferdinand has praised Tanzania’s investment in sports infrastructure, describing the country’s hospitality and commitment to sports development as exceptional. Speaking on May 21 during a visit to the ongoing construction of the Arusha Sports Complex, Ferdinand said he was impressed by the warm reception he had received since arriving in Tanzania, adding that he had rarely experienced such hospitality elsewhere in the world. “ The reception I have received in Tanzania has been truly special. The people are very welcoming, the food is excellent and, overall, Tanzania is a beautiful country,” Ferdinand said. The former football star said every place he had visited in Tanzania was marked by warmth, respect and generosity from local residents, making him feel at home. Ferdinand added that the hospitality he experienced had encouraged him to return to the country and strengthen cooperation with Tanzania in the development of sports. He also commended progress on the construction of the Arusha Sports Complex, describing it as one of the most impressive modern sporting facilities he had seen and a reflection of Tanzania’s commitment to advancing the sports sector. “I have played in many stadiums around the world, but this facility stands out for its quality and modern standards. I congratulate the builders, contractors and all experts involved in implementing this important project,” he said. Ferdinand said he plans to return to Tanzania once the stadium is completed to witness its impact firsthand, noting that investment in modern sports facilities is essential for nurturing talent and promoting the growth of football in the country.

Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo, amesema kuwa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), linatarajia kuanza safari za ndege kuelekea nchini Urusi mnamo Juni, 2026. Ameyasema hayo Mei 15, 2026 jijini Arusha wakati aliposhiriki katika Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Urusi linaloendelea jijini humo katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC). Waziri Mahmoud ameeleza kuwa, nchi ya Urusi inapendelea kupata mazao yenye viwango vya hali ya juu kutoka nchini Tanzania lakini huenda ni ngumu wafanyabiashara kukidhi kigezo hicho kutokana na uhaba wa usafiri wa haraka wa kufikisha bidhaa zikiwa na ubora wake. “Tunalishukuru shirika letu la ndege nchini kwa kukamilisha mikataba yote ambapo ifikapo Juni 2026, safari zitaanza kutoka Tanzania kwenda jijini Moscow na baadaye Saint Petersburg. Wakati ndege hizo zinarudi kutoka kwenye maeneo hayo, tunategemea zitabeba watalii watakaokuja kufanya utalii nchini katika maeneo ya Zanzibar, Kilimanjaro na Dar es Salaam”. Ameongeza kuwa, shirika hilo litakuwa na ndege itakayobeba mizigo hivyo, ametoa rai kwa wafanyabiashara wanaohitaji kusafirisha bidhaa kwa haraka kutumia usafiri huo. Ametaja baadhi ya fursa ambazo Tanzania na Urusi wanaweza kushirikiana ikiwemo ujenzi wa viwanda vya mbolea, vifaa vya kilimo, shughuli za ufungashaji, usindikaji na uhifadhi wa bidhaa, TEHAMA pamoja na dawa za binadamu.