Karibu!

Tunakukaribisha kwenye tovuti rasmi ya Msemaji Mkuu wa Serikali upate taarifa na habari sahihi zenye kuakisi malengo ya Serikali, Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 na matarajio ya Watanzania.

Mawasiliano

Tufuatilie

Na. Timothy Mwakyenda – MAELEZO.  Serikali imebainisha mikakati mipya ya kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani katika mwaka wa fedha 2026/2027, hatua inayolenga kuongeza uwezo wa taifa kujitegemea kiuchumi na kugharamia maendeleo kupitia rasilimali zake. Akizungumza Bungeni jijini Dodoma Juni 11, 2026 wakati akiwasilisha Bajeti ya Serikali ya mwaka 2026/2027, Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, amesema Serikali imejipanga kuongeza kasi ya juhudi za kujitegemea kiuchumi kwa kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani na kuziba mianya yote ya upotevu wa mapato ya Serikali. “Ni muhimu kuendelea kuimarisha uwezo wa nchi kugharamia maendeleo yake kwa kutumia vyanzo vya ndani vya mapato ili kupunguza utegemezi wa mikopo na changamoto zake,” amesema Balozi Omary. Amefafanua kuwa kupitia Mkakati wa Ukusanyaji wa Mapato wa Muda wa Kati wa mwaka 2025/26 hadi 2027/28, Serikali itaanza kutekeleza hatua mbalimbali zitakazopanua wigo wa kodi na kuongeza mapato ya ndani. Miongoni mwa hatua hizo ni kuvutia uwekezaji wa ndani na nje ya nchi ili kuongeza shughuli za kiuchumi, ajira na mapato ya kodi. Serikali pia itaendelea kuhamasisha ulipaji kodi kwa hiari kupitia majukwaa ya mazungumzo kati ya Serikali na sekta binafsi pamoja na kuimarisha matumizi ya mashine za kutolea risiti za kielektroniki (EFD). Aidha, Waziri Omar amesema Serikali itaboresha mifumo ya TEHAMA inayosimamia mapato kwa kutumia teknolojia za kisasa ikiwemo uchambuzi wa taarifa kubwa (Big Data), sambamba na kuunganisha mifumo mbalimbali ya Serikali ili kuongeza uwazi, ufanisi na tija katika ukusanyaji wa mapato. Pia, amesema Serikali itaongeza usimamizi wa taasisi za umma ili ziweze kuchangia zaidi mapato ya Serikali kupitia gawio na michango inayowasilishwa kwa wakati katika Mfuko Mkuu wa Serikali. Katika hatua nyingine, Serikali itaanza kutekeleza baadhi ya mapendekezo 284 yaliyotolewa na Tume ya Rais ya Kuboresha Mfumo wa Kodi. Vilevile, bidhaa zote zinazozalishwa nchini zitatakiwa kuwa na misimbo pau (barcode) kwa lengo la kurahisisha ufuatiliaji wa bidhaa na kudhibiti upotevu wa mapato. Balozi Omar ametangaza pia kuanzishwa kwa programu mpya ya “Tuzo za Uzalendo” itakayozinduliwa rasmi Julai ,2026 kwa lengo la kuhamasisha wananchi kudai risiti na wafanyabiashara kutoa risiti kwa hiari kupitia mfumo wa risiti za kielektroniki na droo za bahati nasibu. Amesema hatua hiyo inalenga kujenga utamaduni wa uzalendo katika ulipaji wa kodi, kuongeza ushiriki wa wananchi katika kulinda mapato ya taifa na kuimarisha uwajibikaji katika shughuli za biashara pia kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato, kupunguza utegemezi wa mikopo na kuimarisha msingi wa uchumi unaojitegemea, shindani na wenye uwezo mkubwa wa kugharamia maendeleo ya wananchi.

Na Scolastica Sambi – MAELEZO Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema ushirikiano kati ya Tanzania na Singapore unafungua ukurasa mpya wa maendeleo ya vijana, uwekezaji na uchumi wa kidijitali, akieleza kuwa Tanzania inalenga kujifunza na kushirikiana na taifa hilo ili kuharakisha safari ya maendeleo ya kizazi kijacho. Akizungumza Ikulu jijini Dar es Salaam, June 9, 2026 baada ya mazungumzo rasmi na Rais wa Singapore, Tharman Shanmugaratnam, Dkt. Samia amesema ziara hiyo ya kihistoria, ambayo ni ya kwanza kufanywa na Rais wa Singapore nchini Tanzania, imekuja wakati muafaka ambapo mataifa hayo mawili yanatimiza miaka 45 ya uhusiano wa kidiplomasia. Rais Samia amesema pamoja na kuimarisha biashara na uwekezaji, viongozi hao wamejadili kwa kina namna ya kuwawezesha vijana wa Tanzania kupitia elimu, mafunzo ya ujuzi, ujasiriamali na ubunifu ili waweze kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kisasa unaotegemea teknolojia na maarifa. “Serikali imeweka kipaumbele kikubwa kwa vijana katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ikiamini kuwa ndani ya miaka 25 ijayo vijana hao ndio watakaokuwa viongozi, wabunifu na watendaji wakuu wa uchumi wa Tanzania” Amesema Rais Samia. Kwa mujibu wa Rais Samia, Tanzania pia imejikita katika utekelezaji wa mkakati wa uchumi wa kidijitali unaolenga kuongeza matumizi ya teknolojia katika uzalishaji, biashara na utoaji wa huduma, huku vijana wakitarajiwa kuwa nguvu kazi kuu ya mageuzi hayo. Aidha, amebainisha kuwa kiwango cha sasa cha biashara kati ya Tanzania na Singapore, kinachofikia dola za Marekani milioni 269 pamoja na miradi 36 ya uwekezaji kutoka Singapore, bado hakilingani na ukubwa wa urafiki uliopo kati ya mataifa hayo mawili. Katika mazungumzo hayo, Tanzania pia imeikaribisha Singapore kuwekeza zaidi katika sekta ya kilimo na usalama wa chakula, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuongeza uzalishaji wa mazao na kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi wenye manufaa kwa pande zote mbili. Rais Samia amesema ujio wa Rais Tharman Shanmugaratnam nchini Tanzania unaashiria mwanzo wa hatua mpya ya ushirikiano wa kimkakati, akisisitiza kuwa kuimarika kwa mahusiano na Singapore, taifa lenye nguvu kubwa kiuchumi duniani, kutachangia kukuza fursa za maendeleo na kuongeza hadhi ya Tanzania katika jukwaa la kimataifa.

MOSCOW, June 3, 2026 — Tanzania and Russia continue to strengthen their diplomatic and economic relationship through high-level discussions aimed at expanding cooperation in trade, tourism, investment, energy, and mineral development. During official talks between Tanzanian President Samia Suluhu Hassan and Russian President Vladimir Putin, both leaders emphasized the importance of deepening cooperation for the mutual benefit of their countries. The discussions focused on increasing trade volumes, attracting investment, and exploring new opportunities in key economic sectors. President Samia highlighted the long-standing relationship between Tanzania and Russia and expressed appreciation for Russia’s historical support during Africa’s liberation movements. “We now have an opportunity to discuss the future development of our countries, but first I must thank Russia for the enormous contribution it made to the liberation of Africa in the 1960s. We have been co-operating with Russia since then and to this day, and Russia has played a huge role in the significant development that we speak about in relation to my country. For this, we are very, very grateful,” President Samia said during the open part of the talks at the Kremlin. The two countries have maintained diplomatic relations for decades and continue to work together on various development initiatives. Recent efforts have included strengthening business partnerships, improving transportation links, and encouraging cooperation in natural resources, education, and tourism.   Economic cooperation remains a major area of interest. Government officials and business representatives from both countries have expressed a commitment to creating a more favorable environment for trade and investment. Areas such as mining, energy, agriculture, and infrastructure development are viewed as having significant potential for future collaboration. Tanzania’s engagement with a wide range of international partners reflects its broader foreign policy approach of promoting economic development through global cooperation. By maintaining relationships with different countries and regions, Tanzania seeks to expand investment opportunities, increase trade, and support national development goals. The growing partnership between Tanzania and Russia highlights the importance of international cooperation in addressing economic challenges and creating opportunities for sustainable growth. As both nations continue to strengthen their ties, they are expected to pursue initiatives that support development, enhance people-to-people relations, and create new opportunities for shared prosperity.  

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa ndege maalum kwa ajili ya kuwachukua mashujaa, Timu ya Taifa ya Vijana U-17 (Serengeti Boys) baada ya kufuzu fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON U-17, 2026. Ndege hiyo imeondoka Juni 01, 2026 inatarajiwa kurejea Jumatano tarehe 3 Juni 2026. Msafara huo umeongozwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda (Mb.), akiambatana na viongozi wa serikali pamoja na Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu (Taifa Stars) ambao watatumia fursa hiyo kushiriki mechi za kirafiki za kimataifa dhidi ya timu zilizopo kwenye kalenda ya FIFA, kama sehemu ya maandalizi ya mashindano yajayo. Aidha, Waziri Makonda amemshukuru Rais Samia kwa kuendelea kuwekeza kwenye michezo na kurahisisha safari hii. Ameziomba familia za Watanzania kuungana kuiombea na kuishangilia Serengeti Boys ili wailetee nchi Kombe la AFCON U-17 na kupeperusha bendera yetu kimataifa.

Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) imetoa rai kwa Watanzania, taasisi za umma na binafsi pamoja na wadau wa maendeleo kuunga mkono harambee maalumu ya kuchangia matibabu ya upandikizaji figo na uloto kwa wagonjwa wenye uhitaji, hususan watoto wenye ugonjwa wa selimundu. Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo, Prof Abel Makubi amesema harambee hiyo ni sehemu ya kilele cha maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa hospitali hiyo mwaka 2015, ambapo lengo ni kukusanya shilingi bilioni saba ndani ya kipindi cha miaka miwili ili kusaidia kuwatibu wananchi wasioweza kumudu gharama za matibabu hayo. Amesema hospitali hiyo imeendelea kukua na kuwa kituo kikubwa cha huduma za kibingwa na ubingwa bobezi nchini, ikiwa na wataalamu wa afya zaidi ya 100 na kutoa huduma 20 za ubingwa pamoja na huduma 18 za ubingwa bobezi. Baadhi ya huduma zinazotolewa ni upasuaji wa moyo, upandikizaji figo, upandikizaji uloto, upasuaji wa ubongo na mishipa ya fahamu, pamoja na huduma nyingine za kisasa zinazopatikana ndani ya nchi. “Tangu kuanza kwa huduma za upandikizaji figo mwaka 2018, jumla ya wagonjwa 56 wamefanyiwa upandikizaji wa figo nchini hatua iliyookoa zaidi ya shilingi bilioni 1.7 ambazo zingetumika kama wagonjwa hao wangetibiwa nje ya nchi”, amesema Prof. Makubi. “Vile vile huduma za upandikizaji uloto kwa watoto wenye ugonjwa wa selimundu zilianza mwaka 2023 ambapo hadi sasa watoto 30 wamefanyiwa upandikizaji huo kwa mafanikio ikiwemo mtoto mmoja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambapo huduma hizo zimeokoa zaidi ya shilingi bilioni 1.3 ambazo zingetumika kwa matibabu nje ya Tanzania”, amemalizia Prof. Makubi. Prof. Makubi ameongeza kuwa licha ya mafanikio hayo, gharama za matibabu ya upandikizaji figo na uloto bado ni kubwa kwa wananchi wengi jambo lililoifanya kuanzisha mfuko maalumu wa kusaidia wagonjwa wenye uhitaji kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF). Kwa niaba ya Hospitali hiyo, Prof. Makubi ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa uwekezaji mkubwa uliofanyika katika sekta ya afya hususan katika kuimarisha huduma za kibingwa na ubingwa bobezi hospitalini hapo.