Karibu!

Tunakukaribisha kwenye tovuti rasmi ya Msemaji Mkuu wa Serikali upate taarifa na habari sahihi zenye kuakisi malengo ya Serikali, Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 na matarajio ya Watanzania.

Mawasiliano

Tufuatilie

Na Baraka Messa – MAELEZO Serikali imekamilisha hatua muhimu za kisheria zitakazowezesha kuanza kwa malipo ya kifuta jasho kwa askari waliojitolea kushiriki Vita ya Kagera dhidi ya utawala wa Idd Amin mwaka 1978/79 ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wao katika kulinda uhuru na usalama wa Taifa. Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba akijibu maswali ya papo kwa papo Juni, 18, 2026, bungeni Dodoma, amesema kuwa vikwazo vya kisheria vilivyokuwa vinazuia utekelezaji wa malipo hayo vimeondolewa kufuatia maelekezo ya Rais, hivyo kufungua njia kwa askari hao kupata stahiki zao baada ya kusubiri kwa muda mrefu. Akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Njombe, Mhe. Deo Mwanyika, Mhe. Waziri Mkuu, amesema kuwa Serikali inaendelea na zoezi la utambuzi na uhakiki wa askari hao, ambapo takribani askari 7,200 wanatarajiwa kunufaika na mpango huo mara baada ya taratibu husika kukamilika. Hatua hii ni sehemu ya dhamira ya Serikali ya kuthamini na kutambua mchango wa wananchi walioweka maisha yao rehani katika nyakati muhimu za historia ya Taifa. Mwaka 2025 Serikali ilikamilisha zoezi la kuwatambua baadhi ya washiriki wa vita hii kutoka Uganda waliokuwa na mchango katika harakati za kuikomboa nchi wakati wa Vita vya Kagera, hatua iliyoweka msingi wa kuendelea kuwathamini wote walioshiriki katika mapambano hayo,” amesema Mhe. Waziri Mkuu. Vita ya Kagera ya mwaka 1978/79 inabaki kuwa moja ya matukio muhimu katika historia ya Tanzania na Afrika Mashariki, ambapo majeshi ya Tanzania kwa kushirikiana na wapigania uhuru wa Uganda yaliweza kuondoa utawala wa Idd Amin na kurejesha usalama katika eneo hilo.  

Na. Mwandishi Wetu – Singida Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba amemuagiza Waziri wa Maji kwenda Mkoa wa Mwanza kushughulikia mara moja changamoto ya upatikanaji wa maji inayowakabili wananchi wa mkoa huo na kuhakikisha huduma hiyo inarejea kwa haraka. Dkt. Mwigulu ametoa maelekezo hayo Juni 14, 2026 alipokuwa akizungumza, kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi wa Tarafa ya Kiomboi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Lulumba, Wilaya ya Iramba mkoani Singida. Amesema amepokea taarifa kuhusu changamoto ya maji katika Mkoa wa Mwanza na tayari amemuelekeza Waziri mwenye dhamana ya maji kwenda eneo husika kusimamia upatikanaji wa suluhisho la haraka.  Nimemtuma Waziri aende haraka Mwanza akasimamie jambo lile mpaka maji yapatikane. Sisi watu wa Singida tunataka tupate maji toka Mwanza. Simiyu tunataka tupate maji toka Mwanza. Dodoma tunataka tupate maji toka Mwanza. Tabora, wengine wameshaanza kupata maji toka Mwanza. Leo kuja kuambiwa Mwanza, pale pale lilipo Ziwa Victoria, pana shida ya maji. Hili ni jambo ambalo haliwezi kueleweka, na wala hatuwezi kulielewa,” amesema Dkt. Mwigulu. Amesema hakuna sababu ya wananchi kuendelea kukosa huduma hiyo wakati chanzo cha maji kinajulikana na miundombinu ya mradi ipo.  “Hatutaki ngonjera za maneno. Hawa wanasema si bomba limekuwaje, hawa wanasema si umeme umekuwaje. Chanzo sisi tunajua kiko pale, hatuna shida ya chanzo cha maji, na mradi upo, na maji yapo. Haya mambo mengine ni ya ngonjera, mimi sitaki kuyasikia,” amesema. Waziri Mkuu amewataka wataalamu wa sekta ya maji pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kufanya kazi kwa pamoja na kuhakikisha wananchi wanapata huduma hiyo kwa haraka. “Mkuu wa Mkoa awatafute wataalamu wake, awatafute TANESCO na wataalamu wa maji. wachimbe kiini cha tatizo na wakeshe mpaka wananchi wapate maji. Kunapopambazuka kesho nipate majawabu kwamba maji yamepatikana,” amesema. Juni 9, 2026, Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA) ilitoa taarifa kwa umma kuhusu upungufu wa huduma ya maji uliosababishwa na hitilafu za umeme zilizokuwa zikijitokeza mara kwa mara. Wakati huohuo, Dkt. Mwigulu amesema Serikali imejipanga kuhakikisha changamoto ya upatikanaji wa maji katika Tarafa ya Kiomboi na maeneo mengine ya Wilaya ya Iramba inapata ufumbuzi wa kudumu kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maji pamoja na uwekezaji mkubwa unaoendelea kufanywa katika sekta hiyo nchini. Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka kipaumbele maalum katika sekta ya maji kwa kutekeleza miradi ya kimkakati inayolenga kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi.  Niwahakikishie kwamba hili ni eneo ambalo Mheshimiwa Rais ameliwekea kipaumbele cha hali ya juu kwa sababu maji ni uhai, maji ni maisha. Tulihangaika kupata chanzo cha uhakika cha maji na sasa kimepatikana, hatua mbalimbali zinaendelea ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma hiyo kwa uhakika,” amesema. Aidha, amesema Serikali inaendelea na utekelezaji wa mpango wa Gridi ya Taifa ya Maji pamoja na kuimarisha uwezo wa uchimbaji wa visima, ujenzi wa mabwawa na upimaji wa vyanzo vya maji ili kukabiliana na changamoto ya maji katika maeneo mbalimbali nchini. Dkt. Mwigulu ambaye pia ni Mbunge wa Iramba Magharibi amesema Serikali inaendelea na usanifu wa barabara ya Kiomboi–Kisiriri–Sibiti kwa lengo la kuijenga kwa kiwango cha lami na kuboresha mawasiliano kati ya wananchi wa maeneo hayo na maeneo jirani. Aidha, amesema usanifu wa barabara ya Kitusha–Galangala–Kisana–Kinampanda–Kisiriri umekamilika, huku Serikali ikiendelea na maandalizi ya utekelezaji wa miradi mingine ya barabara katika Wilaya ya Iramba ili kurahisisha shughuli za kijamii na kiuchumi. Pia amesema usanifu wa daraja la kuunganisha eneo la Hospitali ya Kiomboi na maeneo ya Meli pamoja na Iguguno umekamilika na hatua zinazofuata ni kumpata mkandarasi kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi huo. Sambamba na hilo, Dkt. Mwigulu amesema Serikali inaendelea na maandalizi ya kuanzisha Chuo Kikuu katika eneo la Kiomboi baada ya eneo lililotengwa kuridhiwa na wataalamu husika.  Hapa Kiomboi tutakuwa na Chuo Kikuu. Eneo limekaguliwa na kuridhiwa na hatua za utekelezaji zinaanza,” amesema. Amesema pindi ujenzi wake utakapokamilika, Chuo Kikuu hicho kinatarajiwa kuanza kwa awamu ya kwanza kwa uwezo wa kuhudumia wanafunzi takribani 10,000.

Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imeandika historia nyingine baada ya jopo la madaktari bingwa na wataalamu wa afya kufanikisha salama uzazi wa watoto watano kwa wakati mmoja kwa Bi. Victoria Mkwizu, mkazi wa Tabata jijini Dar es Salaam. Watoto hao ambao watatu ni wa kiume na wawili ni wa kike, wamezaliwa tarehe 13 Juni 2026 na wanaendelea vizuri chini ya uangalizi wa wataalamu wa hospitali hiyo. Akiwa wodini, Bi. Victoria amesema anafurahia huduma alizopata katika hospitali hiyo tangu alipopokelewa hadi kujifungua. “Nawapongeza madaktari, wauguzi na wataalamu wengine wa afya kwa uangalizi wa karibu walionipatia katika kipindi chote cha matibabu kwani mchango wao umetuwezesha mimi na watoto kuendelea vizuri”, amesema Bi. Victoria. Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji, Dkt. Rachel Mhaville amesema tukio hilo ni la kipekee na limehitaji ufuatiliaji wa karibu kutoka kwa timu ya wataalamu wa hospitali hiyo ili kuhakikisha usalama wa mama na watoto huku akimpongeza Bi. Victoria kwa kujifungua salama na kuwatakia wote afya njema. Tunampongeza sana Bi. Veronica kwa kubarikiwa watoto mapacha watano, hospitali yetu itagharamia gharama zote za matibabu za kwake na watoto wake kuanzia alipolazwa hospitalini tarehe 15 Mei, 2026 hadi watakapomaliza matibabu na kuruhusiwa kurejea nyumbani”, ameeleza Dkt. Rachel. Amefafanua kuwa, hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za hospitali kuhakikisha mama na watoto wanaendelea kupata huduma bora na salama katika kipindi hicho.

Na. Timothy Mwakyenda – MAELEZO.  Serikali imebainisha mikakati mipya ya kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani katika mwaka wa fedha 2026/2027, hatua inayolenga kuongeza uwezo wa taifa kujitegemea kiuchumi na kugharamia maendeleo kupitia rasilimali zake. Akizungumza Bungeni jijini Dodoma Juni 11, 2026 wakati akiwasilisha Bajeti ya Serikali ya mwaka 2026/2027, Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, amesema Serikali imejipanga kuongeza kasi ya juhudi za kujitegemea kiuchumi kwa kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani na kuziba mianya yote ya upotevu wa mapato ya Serikali. “Ni muhimu kuendelea kuimarisha uwezo wa nchi kugharamia maendeleo yake kwa kutumia vyanzo vya ndani vya mapato ili kupunguza utegemezi wa mikopo na changamoto zake,” amesema Balozi Omary. Amefafanua kuwa kupitia Mkakati wa Ukusanyaji wa Mapato wa Muda wa Kati wa mwaka 2025/26 hadi 2027/28, Serikali itaanza kutekeleza hatua mbalimbali zitakazopanua wigo wa kodi na kuongeza mapato ya ndani. Miongoni mwa hatua hizo ni kuvutia uwekezaji wa ndani na nje ya nchi ili kuongeza shughuli za kiuchumi, ajira na mapato ya kodi. Serikali pia itaendelea kuhamasisha ulipaji kodi kwa hiari kupitia majukwaa ya mazungumzo kati ya Serikali na sekta binafsi pamoja na kuimarisha matumizi ya mashine za kutolea risiti za kielektroniki (EFD). Aidha, Waziri Omar amesema Serikali itaboresha mifumo ya TEHAMA inayosimamia mapato kwa kutumia teknolojia za kisasa ikiwemo uchambuzi wa taarifa kubwa (Big Data), sambamba na kuunganisha mifumo mbalimbali ya Serikali ili kuongeza uwazi, ufanisi na tija katika ukusanyaji wa mapato. Pia, amesema Serikali itaongeza usimamizi wa taasisi za umma ili ziweze kuchangia zaidi mapato ya Serikali kupitia gawio na michango inayowasilishwa kwa wakati katika Mfuko Mkuu wa Serikali. Katika hatua nyingine, Serikali itaanza kutekeleza baadhi ya mapendekezo 284 yaliyotolewa na Tume ya Rais ya Kuboresha Mfumo wa Kodi. Vilevile, bidhaa zote zinazozalishwa nchini zitatakiwa kuwa na misimbo pau (barcode) kwa lengo la kurahisisha ufuatiliaji wa bidhaa na kudhibiti upotevu wa mapato. Balozi Omar ametangaza pia kuanzishwa kwa programu mpya ya “Tuzo za Uzalendo” itakayozinduliwa rasmi Julai ,2026 kwa lengo la kuhamasisha wananchi kudai risiti na wafanyabiashara kutoa risiti kwa hiari kupitia mfumo wa risiti za kielektroniki na droo za bahati nasibu. Amesema hatua hiyo inalenga kujenga utamaduni wa uzalendo katika ulipaji wa kodi, kuongeza ushiriki wa wananchi katika kulinda mapato ya taifa na kuimarisha uwajibikaji katika shughuli za biashara pia kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato, kupunguza utegemezi wa mikopo na kuimarisha msingi wa uchumi unaojitegemea, shindani na wenye uwezo mkubwa wa kugharamia maendeleo ya wananchi.

Na Scolastica Sambi – MAELEZO Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema ushirikiano kati ya Tanzania na Singapore unafungua ukurasa mpya wa maendeleo ya vijana, uwekezaji na uchumi wa kidijitali, akieleza kuwa Tanzania inalenga kujifunza na kushirikiana na taifa hilo ili kuharakisha safari ya maendeleo ya kizazi kijacho. Akizungumza Ikulu jijini Dar es Salaam, June 9, 2026 baada ya mazungumzo rasmi na Rais wa Singapore, Tharman Shanmugaratnam, Dkt. Samia amesema ziara hiyo ya kihistoria, ambayo ni ya kwanza kufanywa na Rais wa Singapore nchini Tanzania, imekuja wakati muafaka ambapo mataifa hayo mawili yanatimiza miaka 45 ya uhusiano wa kidiplomasia. Rais Samia amesema pamoja na kuimarisha biashara na uwekezaji, viongozi hao wamejadili kwa kina namna ya kuwawezesha vijana wa Tanzania kupitia elimu, mafunzo ya ujuzi, ujasiriamali na ubunifu ili waweze kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kisasa unaotegemea teknolojia na maarifa. “Serikali imeweka kipaumbele kikubwa kwa vijana katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ikiamini kuwa ndani ya miaka 25 ijayo vijana hao ndio watakaokuwa viongozi, wabunifu na watendaji wakuu wa uchumi wa Tanzania” Amesema Rais Samia. Kwa mujibu wa Rais Samia, Tanzania pia imejikita katika utekelezaji wa mkakati wa uchumi wa kidijitali unaolenga kuongeza matumizi ya teknolojia katika uzalishaji, biashara na utoaji wa huduma, huku vijana wakitarajiwa kuwa nguvu kazi kuu ya mageuzi hayo. Aidha, amebainisha kuwa kiwango cha sasa cha biashara kati ya Tanzania na Singapore, kinachofikia dola za Marekani milioni 269 pamoja na miradi 36 ya uwekezaji kutoka Singapore, bado hakilingani na ukubwa wa urafiki uliopo kati ya mataifa hayo mawili. Katika mazungumzo hayo, Tanzania pia imeikaribisha Singapore kuwekeza zaidi katika sekta ya kilimo na usalama wa chakula, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuongeza uzalishaji wa mazao na kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi wenye manufaa kwa pande zote mbili. Rais Samia amesema ujio wa Rais Tharman Shanmugaratnam nchini Tanzania unaashiria mwanzo wa hatua mpya ya ushirikiano wa kimkakati, akisisitiza kuwa kuimarika kwa mahusiano na Singapore, taifa lenye nguvu kubwa kiuchumi duniani, kutachangia kukuza fursa za maendeleo na kuongeza hadhi ya Tanzania katika jukwaa la kimataifa.

MOSCOW, June 3, 2026 — Tanzania and Russia continue to strengthen their diplomatic and economic relationship through high-level discussions aimed at expanding cooperation in trade, tourism, investment, energy, and mineral development. During official talks between Tanzanian President Samia Suluhu Hassan and Russian President Vladimir Putin, both leaders emphasized the importance of deepening cooperation for the mutual benefit of their countries. The discussions focused on increasing trade volumes, attracting investment, and exploring new opportunities in key economic sectors. President Samia highlighted the long-standing relationship between Tanzania and Russia and expressed appreciation for Russia’s historical support during Africa’s liberation movements. “We now have an opportunity to discuss the future development of our countries, but first I must thank Russia for the enormous contribution it made to the liberation of Africa in the 1960s. We have been co-operating with Russia since then and to this day, and Russia has played a huge role in the significant development that we speak about in relation to my country. For this, we are very, very grateful,” President Samia said during the open part of the talks at the Kremlin. The two countries have maintained diplomatic relations for decades and continue to work together on various development initiatives. Recent efforts have included strengthening business partnerships, improving transportation links, and encouraging cooperation in natural resources, education, and tourism.   Economic cooperation remains a major area of interest. Government officials and business representatives from both countries have expressed a commitment to creating a more favorable environment for trade and investment. Areas such as mining, energy, agriculture, and infrastructure development are viewed as having significant potential for future collaboration. Tanzania’s engagement with a wide range of international partners reflects its broader foreign policy approach of promoting economic development through global cooperation. By maintaining relationships with different countries and regions, Tanzania seeks to expand investment opportunities, increase trade, and support national development goals. The growing partnership between Tanzania and Russia highlights the importance of international cooperation in addressing economic challenges and creating opportunities for sustainable growth. As both nations continue to strengthen their ties, they are expected to pursue initiatives that support development, enhance people-to-people relations, and create new opportunities for shared prosperity.  

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa ndege maalum kwa ajili ya kuwachukua mashujaa, Timu ya Taifa ya Vijana U-17 (Serengeti Boys) baada ya kufuzu fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON U-17, 2026. Ndege hiyo imeondoka Juni 01, 2026 inatarajiwa kurejea Jumatano tarehe 3 Juni 2026. Msafara huo umeongozwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda (Mb.), akiambatana na viongozi wa serikali pamoja na Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu (Taifa Stars) ambao watatumia fursa hiyo kushiriki mechi za kirafiki za kimataifa dhidi ya timu zilizopo kwenye kalenda ya FIFA, kama sehemu ya maandalizi ya mashindano yajayo. Aidha, Waziri Makonda amemshukuru Rais Samia kwa kuendelea kuwekeza kwenye michezo na kurahisisha safari hii. Ameziomba familia za Watanzania kuungana kuiombea na kuishangilia Serengeti Boys ili wailetee nchi Kombe la AFCON U-17 na kupeperusha bendera yetu kimataifa.

Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) imetoa rai kwa Watanzania, taasisi za umma na binafsi pamoja na wadau wa maendeleo kuunga mkono harambee maalumu ya kuchangia matibabu ya upandikizaji figo na uloto kwa wagonjwa wenye uhitaji, hususan watoto wenye ugonjwa wa selimundu. Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo, Prof Abel Makubi amesema harambee hiyo ni sehemu ya kilele cha maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa hospitali hiyo mwaka 2015, ambapo lengo ni kukusanya shilingi bilioni saba ndani ya kipindi cha miaka miwili ili kusaidia kuwatibu wananchi wasioweza kumudu gharama za matibabu hayo. Amesema hospitali hiyo imeendelea kukua na kuwa kituo kikubwa cha huduma za kibingwa na ubingwa bobezi nchini, ikiwa na wataalamu wa afya zaidi ya 100 na kutoa huduma 20 za ubingwa pamoja na huduma 18 za ubingwa bobezi. Baadhi ya huduma zinazotolewa ni upasuaji wa moyo, upandikizaji figo, upandikizaji uloto, upasuaji wa ubongo na mishipa ya fahamu, pamoja na huduma nyingine za kisasa zinazopatikana ndani ya nchi. “Tangu kuanza kwa huduma za upandikizaji figo mwaka 2018, jumla ya wagonjwa 56 wamefanyiwa upandikizaji wa figo nchini hatua iliyookoa zaidi ya shilingi bilioni 1.7 ambazo zingetumika kama wagonjwa hao wangetibiwa nje ya nchi”, amesema Prof. Makubi. “Vile vile huduma za upandikizaji uloto kwa watoto wenye ugonjwa wa selimundu zilianza mwaka 2023 ambapo hadi sasa watoto 30 wamefanyiwa upandikizaji huo kwa mafanikio ikiwemo mtoto mmoja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambapo huduma hizo zimeokoa zaidi ya shilingi bilioni 1.3 ambazo zingetumika kwa matibabu nje ya Tanzania”, amemalizia Prof. Makubi. Prof. Makubi ameongeza kuwa licha ya mafanikio hayo, gharama za matibabu ya upandikizaji figo na uloto bado ni kubwa kwa wananchi wengi jambo lililoifanya kuanzisha mfuko maalumu wa kusaidia wagonjwa wenye uhitaji kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF). Kwa niaba ya Hospitali hiyo, Prof. Makubi ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa uwekezaji mkubwa uliofanyika katika sekta ya afya hususan katika kuimarisha huduma za kibingwa na ubingwa bobezi hospitalini hapo.

Na Scolastica Sambi – MAELEZO Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, amewataka Majaji wapya wa Mahakama ya Rufani kuongeza nguvu katika utoaji wa haki nchini na kuwasisitiza kuwa dhamana waliyopewa ni kubwa kwa mustakabali wa Taifa na ustawi wa wananchi. Akizungumza wakati wa kuwaapisha majaji hao, tarehe 26 Mei, 2026, Ikulu Dar es Salaam, Rais, Dkt. Samia amesema uteuzi wao umetokana na uzoefu, weledi pamoja na utumishi mzuri waliouonyesha katika nafasi mbalimbali walizowahi kuzitumikia ndani ya mhimili wa Mahakama.   Amesema hatua ya kupandishwa kwao ni ishara kuwa kazi zao zimetambuliwa na kuthaminiwa na Tume ya Utumishi wa Mahakama, jambo linaloonyesha imani kubwa waliyopewa katika kusimamia haki za Watanzania. “Nendeni mkatumikie nchi kwa uadilifu, weledi na uzalendo kama mlivyoapa hapa. Dhamana hii si ya cheo tu, bali ni wajibu wa kulinda haki za wananchi,” amesema Rais Samia. Katika hotuba yake, Rais Samia amesema kazi ya jaji ni miongoni mwa majukumu yenye uzito mkubwa katika jamii kwa sababu ndiyo yanayogusa moja kwa moja maisha, haki na matumaini ya wananchi. “Ukimuacha Mungu anayesimamia haki za wote, basi wengine aliowateua kusimamia haki za wananchi ni ninyi majaji. Hivyo mnafanya kazi yenye dhamana kubwa kwa Taifa,” amesisitiza. Aidha, aliwataka majaji hao kuhakikisha wanaitunza heshima na uhuru wa mahakama kwa kutoa maamuzi yanayozingatia sheria, haki pamoja na maslahi mapana ya Taifa, huku akieleza kuwa Mahakama ya Rufani ndiyo ngazi ya juu kabisa ya utoaji haki nchini. Rais Samia ameongeza kuwa Serikali itaendelea kuimarisha mhimili wa mahakama kupitia maboresho mbalimbali ili kuhakikisha taasisi hiyo muhimu inaendelea kutoa haki kwa ufanisi, weledi na kwa wakati.

By Baraka Messa – MAELEZO Former Manchester United and England defender Rio Ferdinand has praised Tanzania’s investment in sports infrastructure, describing the country’s hospitality and commitment to sports development as exceptional. Speaking on May 21 during a visit to the ongoing construction of the Arusha Sports Complex, Ferdinand said he was impressed by the warm reception he had received since arriving in Tanzania, adding that he had rarely experienced such hospitality elsewhere in the world. “ The reception I have received in Tanzania has been truly special. The people are very welcoming, the food is excellent and, overall, Tanzania is a beautiful country,” Ferdinand said. The former football star said every place he had visited in Tanzania was marked by warmth, respect and generosity from local residents, making him feel at home. Ferdinand added that the hospitality he experienced had encouraged him to return to the country and strengthen cooperation with Tanzania in the development of sports. He also commended progress on the construction of the Arusha Sports Complex, describing it as one of the most impressive modern sporting facilities he had seen and a reflection of Tanzania’s commitment to advancing the sports sector. “I have played in many stadiums around the world, but this facility stands out for its quality and modern standards. I congratulate the builders, contractors and all experts involved in implementing this important project,” he said. Ferdinand said he plans to return to Tanzania once the stadium is completed to witness its impact firsthand, noting that investment in modern sports facilities is essential for nurturing talent and promoting the growth of football in the country.